mi kweli natamani siku iwezekane
mi kweli natamani siku iwezekane
mara nyingi peke yangu nawaza
namuomba mungu nisije kukwaza
nikaja kukupa maudhi na nafsi kuichoma
chei! tena usiku mzima nalia darling
napiga goti kwa mola nasali
azidi tupe baraka tusije kosa dona
nimejaliwa mboni lakini nuru sina
ningefanya kazi nikuhudumie
upofu wangu ndio kikwazo kikubwa
mbali na mengi unanipenda sana
mi kweli natamani siku iwezekane
mi kweli natamani siku iwezekane
nasikia kuna rangi ya upendo
ili upendwe kuna pozi za mwendo
udambudambu na urembo mi sina
kwa ardhi na mbingu nilalame
nipande mawingu na niliname
nimejaliwa mboni lakini nuru sina
ningefanya kazi nikuhudumie
upofu wangu ndio kikwazo kikubwa
mbali na mengi unanipenda sana
mi kweli natamani siku iwezekane
mi kweli natamani siku iwezekane